Zana na vidokezo vya kukusaidia
uwe salama mtandaoni.

Tunalinda faragha yako kiotomatiki kwa kutumia mbinu bora zaidi za usalama. Kuna hatua chache za ziada unazoweza kuchukua ili udhibiti usalama wako mtandaoni na uchague kiwango sahihi cha ulinzi unaokufaa.

Imarisha usalama
wa Akaunti yako ya Google.

Ukaguzi wa Usalama

Kagua Usalama

Njia rahisi ya kulinda Akaunti yako ya Google ni kufanya Ukaguzi wa Usalama. Zana hii ya hatua kwa hatua inakupatia mapendekezo mahususi yanayokufaa, yenye hatua unazoweza kuchukua ili uimarishe usalama wa Akaunti yako ya Google.

UTHIBITISHAJI WA HATUA MBILI

Jilinde dhidi ya wadukuzi ukitumia Uthibitishaji wa Hatua Mbili

Uthibitishaji wa Hatua Mbili husaidia kumzuia mtu yeyote ambaye hastahili kufikia akaunti yako kwa kukuomba utumie njia ya pili kando na jina la mtumiaji na nenosiri ili kuingia katika akaunti. Kwa watu walio katika hatari ya kulengwa na mashambulizi mahususi ya mtandaoni na wanahitaji ulinzi thabiti zaidi, tumebuni Mpango wa Ulinzi wa Hali ya Juu.

Usaidizi kiasi katika
ulinzi wa manenosiri yako.

Tumia manenosiri thabiti na ya kipekee

Kutunga nenosiri thabiti na maalum kwa kila akaunti ni mojawapo ya hatua muhimu zaidi unayoweza kuchukua ili kulinda faragha yako. Hatua ya kutumia nenosiri lile lile kuingia katika akaunti nyingi, kama vile akaunti ya Google, wasifu wa mitandao jamii na tovuti za wauzaji, huhatarisha usalama.

Fuatilia manenosiri yako yote

Kidhibiti cha manenosiri kama kile kilichojumuishwa kwenye Akaunti yako ya Google, husaidia kulinda na kufuatilia manenosiri unayotumia kwenye tovuti na programu. Kidhibiti cha Manenosiri cha Google kinakusaidia kutunga, kukumbuka na kuhifadhi manenosiri yako yote kwa usalama ili uweze kuingia katika akaunti zako kwa njia rahisi na salama.

Kagua manenosiri yako ili uone kama kuna matatizo ya usalama

Kagua uthabiti na usalama wa manenosiri yako yote uliyohifadhi kwa kufanya Ukaguzi wa Manenosiri kwa haraka. Fahamu iwapo manenosiri yako yoyote uliyohifadhi ya akaunti au tovuti za wengine yameathiriwa na uyabadilishe kwa urahisi panapohitajika.

Tumia manenosiri thabiti na ya kipekee

Kutunga nenosiri thabiti na maalum kwa kila akaunti ni mojawapo ya hatua muhimu zaidi unayoweza kuchukua ili kulinda faragha yako. Hatua ya kutumia nenosiri lile lile kuingia katika akaunti nyingi, kama vile akaunti ya Google, wasifu wa mitandao jamii na tovuti za wauzaji, huhatarisha usalama.

Fuatilia manenosiri yako yote

Kidhibiti cha manenosiri kama kile kilichojumuishwa kwenye Akaunti yako ya Google, husaidia kulinda na kufuatilia manenosiri unayotumia kwenye tovuti na programu. Kidhibiti cha Manenosiri cha Google kinakusaidia kutunga, kukumbuka na kuhifadhi manenosiri yako yote kwa usalama ili uweze kuingia katika akaunti zako kwa njia rahisi na salama.

Kagua manenosiri yako ili uone kama kuna matatizo ya usalama

Kagua uthabiti na usalama wa manenosiri yako yote uliyohifadhi kwa kufanya Ukaguzi wa Manenosiri kwa haraka. Fahamu iwapo manenosiri yako yoyote uliyohifadhi ya akaunti au tovuti za wengine yameathiriwa na uyabadilishe kwa urahisi panapohitajika.

Pata maelezo zaidi kuhusu Kidhibiti cha Manenosiri cha Google
Linda usalama wa vifaa vyako.
Vinjari mtandaoni kwa usalama.
Simu inayoangazia arifa inayoonyesha kuwa muunganisho ni salama
Epuka ulaghai wa mtandaoni na
majaribio ya wizi wa data binafsi

Fahamu jinsi unavyoweza kulaghaiwa

Walaghai hutumia fursa ya nia njema kwa kufanya ulaghai wao uonekane kama ujumbe halali. Kando na barua pepe, walaghai wanaweza pia kutumia ujumbe wa maandishi, simu zinazopigwa kiotomatiki na tovuti hasidi ili kukulaghai.

Thibitisha kila wakati viungo au URL unazotilia shaka

Wizi wa data binafsi ni jaribio la kukuhadaa ili utoe taarifa muhimu ya binafsi au ya kifedha, kama vile nenosiri au maelezo ya benki. Unaweza kutekelezwa kwa njia nyingi, kama vile ukurasa bandia wa kuingia katika akaunti. Ili kuepuka wizi wa data binafsi, usiwahi kubofya viungo unavyotilia shaka; hakikisha usalama wa URL — kwa kufanya kiashiria chako kielee juu ya kiungo au kubonyeza kwa muda mrefu maandishi yaliyo kwenye kifaa chako cha mkononi — ili uhakikishe kuwa programu au tovuti ni halali; na uhakikishe kuwa URL inaanza kwa “https.”

Tahadhari dhidi ya waigaji

Walaghai wanaweza kujifanya kuwa mashirika halali kama vile serikali au mashirika yasiyo ya faida. Tahadhari kila wakati unaposoma ujumbe kutoka kwa mtu anayedai kuwa ana mamlaka fulani. Ikiwa mtu unayemjua atakutumia barua pepe, lakini ujumbe huo uwe si wa kawaida, inamaanisha kuwa huenda akaunti yake imedukuliwa. Usijibu ujumbe au ubofye viungo vyovyote isipokuwa uwe unaweza kuthibitisha kuwa barua pepe ni halali. Chunguza vitu kama vile maombi ya dharura ya pesa, habari za kusikitisha kuwa mtu anateseka ughaibuni na anahitaji usaidizi au mtu anayedai kuwa simu yake imeibwa na hawezi kupatikana kwenye simu.

Tahadhari dhidi ya ulaghai kupitia barua au maombi ya taarifa binafsi

Ujumbe kutoka kwa watu usiowajua unaweza kushukiwa na hata mawasiliano kutoka kwa mtu unayemwani, kama vile benki yako, yanaweza kuwa uigaji. Usijibu barua pepe, ujumbe wa papo hapo au madirisha ibukizi unayotilia shaka, ambayo yanakuomba taarifa binafsi. Usiwahi kubofya viungo unavyotilia shaka au kuweka taarifa binafsi kwenye utafiti au fomu unazoshuku. Ukiombwa utoe msaada kwa shirika lisilo la faida, nenda moja kwa moja kwenye tovuti ya shirika hilo ili utoe mchango wako badala ya kubofya kiungo ulichotumiwa.

Thibitisha faili kabla ya kuzipakua

Baadhi ya wizi wa data binafsi unaweza kutokea kupitia viambatisho vya PDF na hati zilizoathiriwa. Ukipata kiambatisho unachotilia shaka, tumia Chrome au Google Drive kukifungua. Tutachanganua moja kwa moja faili hiyo na kukuonya tukitambua kuwa ina virusi.

Fahamu jinsi unavyoweza kulaghaiwa

Walaghai hutumia fursa ya nia njema kwa kufanya ulaghai wao uonekane kama ujumbe halali. Kando na barua pepe, walaghai wanaweza pia kutumia ujumbe wa maandishi, simu zinazopigwa kiotomatiki na tovuti hasidi ili kukulaghai.

Thibitisha kila wakati viungo au URL unazotilia shaka

Wizi wa data binafsi ni jaribio la kukuhadaa ili utoe taarifa muhimu ya binafsi au ya kifedha, kama vile nenosiri au maelezo ya benki. Unaweza kutekelezwa kwa njia nyingi, kama vile ukurasa bandia wa kuingia katika akaunti. Ili kuepuka wizi wa data binafsi, usiwahi kubofya viungo unavyotilia shaka; hakikisha usalama wa URL — kwa kufanya kiashiria chako kielee juu ya kiungo au kubonyeza kwa muda mrefu maandishi yaliyo kwenye kifaa chako cha mkononi — ili uhakikishe kuwa programu au tovuti ni halali; na uhakikishe kuwa URL inaanza kwa “https.”

Tahadhari dhidi ya waigaji

Walaghai wanaweza kujifanya kuwa mashirika halali kama vile serikali au mashirika yasiyo ya faida. Tahadhari kila wakati unaposoma ujumbe kutoka kwa mtu anayedai kuwa ana mamlaka fulani. Ikiwa mtu unayemjua atakutumia barua pepe, lakini ujumbe huo uwe si wa kawaida, inamaanisha kuwa huenda akaunti yake imedukuliwa. Usijibu ujumbe au ubofye viungo vyovyote isipokuwa uwe unaweza kuthibitisha kuwa barua pepe ni halali. Chunguza vitu kama vile maombi ya dharura ya pesa, habari za kusikitisha kuwa mtu anateseka ughaibuni na anahitaji usaidizi au mtu anayedai kuwa simu yake imeibwa na hawezi kupatikana kwenye simu.

Tahadhari dhidi ya ulaghai kupitia barua au maombi ya taarifa binafsi

Ujumbe kutoka kwa watu usiowajua unaweza kushukiwa na hata mawasiliano kutoka kwa mtu unayemwani, kama vile benki yako, yanaweza kuwa uigaji. Usijibu barua pepe, ujumbe wa papo hapo au madirisha ibukizi unayotilia shaka, ambayo yanakuomba taarifa binafsi. Usiwahi kubofya viungo unavyotilia shaka au kuweka taarifa binafsi kwenye utafiti au fomu unazoshuku. Ukiombwa utoe msaada kwa shirika lisilo la faida, nenda moja kwa moja kwenye tovuti ya shirika hilo ili utoe mchango wako badala ya kubofya kiungo ulichotumiwa.

Thibitisha faili kabla ya kuzipakua

Baadhi ya wizi wa data binafsi unaweza kutokea kupitia viambatisho vya PDF na hati zilizoathiriwa. Ukipata kiambatisho unachotilia shaka, tumia Chrome au Google Drive kukifungua. Tutachanganua moja kwa moja faili hiyo na kukuonya tukitambua kuwa ina virusi.

Gundua njia zaidi tunazotumia
kulinda usalama wako mtandaoni.