Njia salama zaidi ya kuingia katika akaunti zako zote za mtandaoni.
Kwenye akaunti zako zote za mtandaoni, hatua ya kuingia katika akaunti ni njia ya kwanza ya kufikia taarifa zako binafsi. Pia, ni njia ya msingi ya kupata hatari, kwa hivyo ni muhimu kuilinda.
Tunalinda usalama wa kuingia katika akaunti yako ya Google na huduma na programu zako zote kwa chaguomsingi. Kwa kutumia zana zilizojumuishwa na ulinzi wa kiotomatiki, kama vile kukutumia arifa Akaunti yako ya Google inapofikiwa kwenye kifaa kipya, tunafanya iwe rahisi na haraka kuingia katika akaunti kwa usalama.
-
Manenosiri thabiti husaidia kudumisha usalama wako
Kuweka manenosiri thabiti na maalum kwenye akaunti zako za mtandaoni ni hatua muhimu katika kudumisha faragha ya taarifa zako binafsi, lakini watu wengi husema kuwa wanatumia manenosiri sawa ambayo ni dhaifu kwenye tovuti nyingi, hali ambayo huongeza uwezekano wa kuathiriwa kwa akaunti hizo.
-
Kidhibiti Manenosiri kutoka Google hukusaidia utunge manenosiri thabiti
Dhibiti Manenosiri uliyohifadhiKipengele cha Kidhibiti Manenosiri kilichojumuishwa kwenye Chrome na Android, hutunga, kuhifadhi kwa usalama na kuweka manenosiri kiotomatiki kwenye akaunti zako zote za mtandaoni.
-
Arifa Otomatiki kuhusu Manenosiri husaidia kulinda usalama wa manenosiri yako
Kila siku, matukio mapya ya ufichuzi haramu wa data hufichua majina ya watumiaji na manenosiri mengi mno. Google hufuatilia ili kubaini manenosiri yaliyoathiriwa. Kwa hivyo, ikiwa mojawapo ya manenosiri uliyohifadhi litapatikana kuwa limefichuliwa kwa njia haramu, tutakuarifu kiotomatiki.
-
Sasisha manenosiri yako kwa kutumia programu ya Mratibu wa Google
TUNAKULETEA HIVI KARIBUNIKuhusu suala la kurekebisha manenosiri yaliyoathiriwa, kuchukua hatua ya haraka zaidi ni muhimu. Chrome iko katika mchakato wa kusambaza kipengele cha kurekebisha haraka: Kinaweza kuripoti manenosiri yako yaliyoathiriwa na kuyabadilisha kwa niaba yako kwa usaidizi wa programu ya Mratibu wa Google, kwa kugusa mara moja.
-
Uthibitishaji wa hatua mbili unatoa hatua ya pili ya usalama wa kuingia katika akaunti
Washa kipengele cha Uthibitishaji wa hatua mbiliKuathiriwa kwa manenosiri ni jambo la kawaida zaidi kuliko jinsi unavyofikiria. Mojawapo ya njia bora zaidi za kulinda akaunti yako ni kuwa na njia ya ziada ya uthibitishaji. Uthibitishaji wa hatua mbili husaidia kuzuia mtu yeyote ambaye hapaswi kufikia akaunti yako kwa kuhitaji hatua ya pili ya uthibitishaji baada ya kuweka nenosiri lako.
-
Uthibitishaji kupitia simu ni rahisi na salama
Hatua ya kutumia kitu halisi cha uthibitishaji unapoingia kwenye akaunti zako za mtandaoni, kama vile simu yako, imethibitishwa kuwa salama zaidi kuliko nenosiri, ambalo linaweza kuathiriwa kwa urahisi. Hii ndiyo sababu tuko katika mstari wa mbele kubuni njia mbadala za uthibitishaji. Kwa kutumia Kidokezo cha Google, utathibitisha akaunti yako kwa kugusa mara moja tu.
-
Kurahisisha zaidi ulinzi wa usalama wa akaunti
Tunabuni pia teknolojia za usalama wa kina kwenye vifaa – kama vile funguo za usalama kwenye Android na programu ya Google Smart Lock kwenye iOS – ili kurahisisha utaratibu wa uthibitishaji na kufanya uwe salama zaidi kuliko matumizi ya nenosiri. Hivi karibuni, tutaanza kuandikisha watumiaji kiotomatiki kwenye huduma ya Uthibitishaji wa Hatua Mbili ikiwa wana anwani ya barua pepe au nambari ya simu ya kurejesha akaunti kwenye akaunti zao. Kagua akaunti yako kwa kutumia Ukaguzi wa Usalama.
-
Njia salama zaidi ya kuingia kwenye huduma na programu uzipendazo
Unapoingia katika akaunti zako za mtandaoni, unapaswa kufanya hivyo kwa usalama na bila taabu. Unaweza kutumia Akaunti yako ya Google kuingia katika tovuti na huduma nyingi kwenye wavuti kwa urahisi na kwa usalama zaidi, huku ukiweka chaguo wazi za faragha katika sehemu moja.
-
Ingia kwenye akaunti kwa usalama popote ulipo, kwa kugusa mara moja tu
Tunachanganya mbinu bora zaidi za usalama kutoka Google na teknolojia rahisi zaidi ili kusaidia kulinda taarifa zako binafsi kwenye akaunti zingine. Kipengele cha Ingia ukitumia akaunti ya Google hukuthibitisha kwa njia maalum kwenye kila huduma. Kwa hivyo, hata kama tukio la ufichuzi haramu wa data litatokea kwenye tovuti au huduma yoyote unayotumia, taarifa zako binafsi kwenye akaunti zingine zote zitalindwa dhidi ya wadukuzi.
-
Udhibiti zaidi wa akaunti na miunganisho yako
Washa kipengele cha Ingia ukitumia akaunti ya GoogleUnaweza kukagua na kudhibiti jinsi unavyotumia kipengele cha Ingia ukitumia akaunti ya Google moja kwa moja kwenye Akaunti yako ya Google. Kinakuruhusu udhibiti au ubatilishe idhini ya ufikiaji wa akaunti yoyote iliyounganishwa — yote katika sehemu moja — hali ambayo inakupa udhibiti kamili.
Linda Akaunti yako ya Google kwa kufanya Ukaguzi wa Usalama. Zana hii ya hatua kwa hatua inakupatia mapendekezo mahususi yanayokufaa, yenye hatua unazoweza kuchukua ili uimarishe usalama wa Akaunti yako ya Google.
kuimarisha usalama wako mtandaoni.
-
Vidhibiti vya faraghaChagua mipangilio ya faragha inayokufaa.
-
Kanuni za dataPata maelezo zaidi kuhusu jinsi tunavyoheshimu faragha yako kwa kutumia kanuni za data.
-
Vidokezo vya usalamaGundua vidokezo vya haraka na desturi bora za kuwa salama mtandaoni.
-
Matangazo na dataPata maelezo zaidi kuhusu matangazo unayoonyeshwa kwenye mifumo yetu.